• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waziri Bashungwa ataka Michezo ya SHIMIWI kuboreshwa.

Posted on: November 3rd, 2021

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa (Mb) ameitaka Mikoa yote nchini na Halmashauri zake kufanya ukarabati wa miundombinu ikiwa ni pamoja na viwanja vya michezo ili viweze kutumika katika michuano ya michezo inayoshrikisha Wizara, Taasisi na Idara za Serikali – SHIMIWI ambayo hufanyika kila mwaka katika Mkoa uliochaguliwa.

Waziri Bashungwa ametoa agizo hilo Oktoba  2 mwaka huu wakati akihitimisha kilele cha michezo ya SHIMIWI iliyofanyika katika uwanja wa Jamhuri katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mkoani humo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akivalishwa Scarf  na Mwenyekiti wa SHIMIWI Taifa Daniel Zacharia kabla ya kuanza kutoa zawadi kwa washindi wa mashindano hayo.

Amesema, Mikoa na Halmashauri zote nchini zinatakiwa kufanya ukarabati wa Miundombinu kama viwanja vya michezo ili michezo itakayoandaliwa na Wizara yake katika Mkoa husika isiwepo changamoto yoyote ya kukwamisha michezo  hiyo kufanyika kwa kisingizio cha miundombinu mibovu.

Aidha, Waziri Bashungwa alitumia jukwaa hilo kumshukuru Mhe. Samia Suluhu Hasaan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kurejesha michezo ya SHIMIWI ambayo ilikuwa imesimamishwa kwa miaka mitano iliyopita.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Bi. Mariam Mtunguja (kushoto) akipokea moja kati ya zawadi za vikombe walivyoshinda timu ya RAS MOROGORO.

Sambamba na hayo Waziri amemhakikishia Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango kutekeleza agizo alilolitoa Oktoba 23 mwaka huu wakati akizindua mashindano hayo  kutathmini Taasisi, Wizara na Idara za Serikali ambazo hazikushiriki michezo hiyo na kwamba taarifa ya tathmini hiyo itawasilishwa katika Ofisi yake mara tu itakapokamilika.

Kwa upande wa changamoto zilizojitokeza kwa wanamichezo juu ya sintofahamu kwa washiriki wa michezo hiyo, Mhe. Bashungwa ametoa onyo kwa Viongozi wa SHIMIWI kutenda haki, na kuratibu vema michezo hiyo ili iwe huru na haki na kwamba Wizara yake itahakikisha inasimamia suala hilo ili kuondoa manung’uniko miongoni mwa wachezaji.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela ameipongeza Serikali kwa kuruhusu mashindano hayo kufanyika katika Mkoa huo licha ya Mikoa mingi  iliyopo hapa nchini lakini Mkoa wa Morogoro uliteuliwa kuwa Mwenyeji wa mashindano hayo.

Sambamba na hayo, Shigela amebainisha mafanikio yaliyotokana na michezo ya SHIMIWI kwa kipindi cha wiki mbili za mashindano hayo ambapo amesema wingi wa wachezaji walioshiriki michezo hiyo umechangia kukuza uchumi wa wafanyabiashara na maendeleo ya Mkoa na taifa kwa jumla.

‘’…Tunasema asanteni sana ndugu zangu kwa kuja katika Mkoa wa Morogoro , uwepo wenu na ushiriki wenu tunauthamini, tutauenzi na kuuweka kwenye kumbukumbu kama watu muhimu mliochangia maendeleo katika Mkoa wa Morogoro.…’’ amesema Shigela.

Naye Mwenyekiti wa SHIMIWI Taifa Daniel Zacharia amemuomba Mhe. Bashungwa kwamba zoezi la kushiriki michezo kwa watumishi wa Umma litekelezwe kwa mujibu wa sheria kutokana na takwimu kuonesha kuwa ushiriki wa Watumishi hao katika mashindano kunawajengea Afya Imara, Nidhamu, urafiki kuongeza ushirikiano, na kudumisha demokrasia na ufanisi wa kazi mahala pa kazi.

 Mashindano haya ya 35 ya SHIMIMI yalianza Oktoba 20 mwaka huu na kuzinduliwa rasmi Oktoba 23 mwaka huu katika uwanja wa Jamhuri Mjini Morogoro na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.  Philip Isdor Mpango yakihusisha timu 47 ambapo jumla ya wachezaji 1,830 walishiriki.

Baadhi ya wachezaji wa timu ya mpira wa miguu TAMISEMI ambao waliibuka kinara katika mpira huo.

Mashindano ya mwaka huu yamehitimishwa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa (Mb) Novemba 2, 2021 ambaye alikuwa mgeni rasmi na kufanikiwa kugawa zawadi kwa timu ambazo zimefanya vizuri.

Kaulimbiu ya michezo hiyo ya SHIMIWI ilikuwa Michezo huleta Afya na ufanisi mahala pa kazi, jihadhari na UVIKO 19 chukua hatua nenda kachanje.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.