• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waziri Kijaji atoa agizo kufuatilia kupanda kwa bei ya saruji baadhi ya Mikoa

Posted on: September 15th, 2023

Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji ameiagiza tume ya Ushindani ya wizara hiyo kufuatilia kinachosababisha bei ya saruji kupanda katika baadhi ya Mikoa hasa katika Mikoa ya Kagera na Mwanza ili waweze kutatua changamoto hiyo.

Waziri Kijaji ametoa maagizo hayo leo Septemba 15, 2023 wakati wa Mkutano wake na waandishi wa Habari uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwa lengo la kutoa taarifa ya hali ya upatikanaji wa bidhaa hapa Nchini.

Amesema anatambua kuwa kuna changamoto ya nishati ya mafuta inayosababisha kwa namna moja ama nyingine kupandisha bei ya bidhaa hiyo ya saruji, hata hivyo amebainisha kuwa sio kwa kiwango ambacho bidhaa hiyo inauzwa.

“Naomba niwaelekeze tume yetu ya ushindani sasa iweze kupita kwenye maeneo yote na hasa Mikoa yetu ya pembezoni wapite na kuona bei ya Saruji ikoje kwa sasa kipi kinachosababisha bei ya saruji kuwa juu zaidi kuliko mikoa mingine...” amesema Dkt. Kijaji.

Sambamba na hilo amewataka wananchi kuuza mazao ya ziada waliyoyapata mwaka huu na kubakiza kwa ajili ya chakula kitakachotosheleza msimu mzima ili kuepuka baadae kununua chakula hicho kwa bei kubwa zaidi kuliko bei ya sasa.

Aidha, amewatahadharisha wafanyabiashara kuhusu Makampuni yanayowalaghai wafanyabiashara na Wananchi kuwa yanatoa kiasi cha fedha kama sehemu ya gharama za kujisajili ili waweze kushiriki katika ziara za kibiashara nje ya nchi na kwamba hao ni matapeli.

“niwaombe Wafanyabiashara na wenye viwanda nchini tunapoyaona matangazo haya kabla ya kufanya chochote ni vyema ukajiridhisha kwa kupata taarifa za fursa hizi kutoka kwenye Mamlaka za Serikali ikiwemo Taasisi yetu ya Maendeleo ya Biashara (Tantrade) ambao ndiyo Taasisi yenye Mamlaka kisheria ya kuratibu masuala yote yanayohusu Maonesho na misafara ya kibiashara iwe ndani au nje ya Nchi yetu”. amesema Dkt. Kijaji.


Mbali na hayo, Waziri ametoa rai kwa wazalishaji wa bidhaa zote za viwandani kuendelea kuongeza jitihada za uzalishaji wa bidhaa wanazozizalisha kwa kuzingatia ubora unaohitajika sokoni na kwa kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu zilizowekwa ili kukabiliana na kupanda kwa bei za bidhaa mbalimbali nchini.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Malima amesema kwa kutumia mfumo wa stakabadhi Ghalani utasaidia wananchi kutatua changamoto ya bei ya mazao kutokana na baadhi ya wafanyabiashara kuwalaghai wakulima kuuza mazao yao kwa bei ya chini yakiwa bado shambani suala ambalo Mkuu wa Mkoa amekemea kuwa ni kumnyonya mkulima.

Kwa sababu hiyo Mkuu wa MKoa bado anatoa ushauri kwa wakulima kuendelea kutumia kuuza mazao yao kupitia mfumo huo wa Stakabadhi ghalani kwa kuwa ndio pekee utakaowanufaisha na kuwakomboa katika kilimo.

Awali, akimkaribisha Waziri kwenye mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Malima alimueleza Waziri juu ya hali ya viwanda vya sukari Mkoani humo kuwa kiwanda cha Kilombero kinachopanuliwa na kiwanda cha Mkulazi kinachojengwa, vyote vinatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Julai mwakani na kwamba vitakapoanza uzalishaji, kwa pamoja vitazalisha jumla ya tani 200,000 kwa mwaka.

Waziri Dkt. Kijaji amefanya mkutano huo na wanahabari ikiwa ni Utaratibu wa kawaida kwa Wizara hiyo unaofanyika kila mwezi tarehe 15 kwa lengo la kudhibiti bei za bidhaa na kutoa taarifa ya bei halisi za bidhaa kwa wananchi.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.