• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAZIRI JAFFO ATOA MAAGIZO KWA UONGOZI MKOA WA MOROGORO.

Posted on: June 18th, 2022

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Dkt. Suleiman Jaffo ameuagiza uongozi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuunda tume maalum ili kuchunguza thamani ya fedha iliyotumika katika ujenzi wa Mradi wa Skimu ya umwagiliaji ya Lukenge Wilayani Mvomero pamoja na kuchunguza maendeleo ya mradi huo na kuwasilisha kwake  taarifa ya uchunguzi huo ndani ya mwezi mmoja.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Dkt. Suleiman Jaffo akitoa maelekezo kwa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuunda tume kuchunguza mradi wa Skimu ya Lukenge Juni 17 Mwaka huu.


Dtk. Suleiman Jaffo ametoa agizo hilo Juni 17 Mwaka huu wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo inayosimamiwa na wizara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro Kata ya Mtibwa Kijiji cha Lukenge.

Dkt. Suleiman Jaffo ameonesha kutokuridhishwa na utekelezaji wa Mradi huo wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi kwa kutumia mifumo ya Kiikolojia Vijijini - EBARR.

Mradi huo uliogharimu zaidi ya shilingi 600Mil. ulikuwa unasimamiwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji NIRC kwa utekelezaji huo ambapo umekuwa wa kusuasua tangu mwaka 2012 hadi sasa.


Mfereji wa Skimu ya Lukenge ambao bado haujakamilika ujenzi na uliotembelewa wakati wa ziara ya Dkt. Suleiman Jaffo Juni 17 mwaka huu.


Aidha, Dkt. Jaffo amesema, kusuasua kwa mradi huo kunawanyima wananchi zaidi 3000 wa kijijini Cha Lukenge kunufaika nao ambao wanajishughulisha na kilimo cha hekta zaidi ya 1000, ambapo tija kubwa ya mazao yao yanategemea ukamilishwaji wa mradi huo.

“Nimekuja kuangalia thamani ya fedha katika mradi huu, sijaridhishwa kabisa na utekelezaji wake na hivyo nielekeze kwa uongozi wa Mkoa wa Morogoro kuunda tume maalum ili kuchunguza na kukagua maendeleo ya mradi huu kisha kuniletea taarifa ndani ya mwezi mmoja” ameagiza Dkt. Jaffo.



Katika hatua nyingine Dkt. Jaffo amekagua na kuridhishwa na utekelezaji wa Mradi wa EBARR wa kilimo cha umwagiliaji uliogharimu zaidi Tsh. 68Mil. unaotekelezwa katika Kata ya Lubungo Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Kijiji cha Mingo ambapo pamoja na mambo mengine amewaagiza wanaotekeleza mradi huo kukamilisha mradi huo kabla au ifikapo Juni 30 mwaka huu.



Naye Mwenyekiti wa Skimu ya Lukenge Bw. Hashim Omary akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo amebainisha changamoto zilizokwamisha mradi huo ikiwemo kutopatikana fedha kwa wakti hali inayopelekea kasi ya ujenzi wa mradi kuwa ndogo.






Kwa upande wake Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya hiyo na mratibu wa mradi huo Bw. Mteri Baraka ameweka bayana kuwa uwajibikaji mdogo na ukosefu wa watumishi wa Tume ya Umwagiliaji Tanzania ni sababu nyingine ya kusuasua kwa mradi hadi sasa, hivyo kumuahidi Waziri Suleiman Jaffo kutekeleza maagizo yote aliyoyatoa kwa ufanisi.

Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Bw. Mteri Baraka akitoa maelezo mbele ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano Dkt. Suleiman Jaffo juu ya maendeleo ya mradi Skimu ya Umwagiliaji ya Lukenge.




MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.