• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Shamba la malisho la hekari 4000 lazinduliwa Kilosa, Waziri Kijaji, RC Malima wasisitiza wakulima, wafugaji kuheshimiana

Posted on: January 4th, 2025



Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (MB) amezindua shamba la hekari 4000 litakaloendelezwa kwa ajili ya malisho ya mifugo ili kuwa na mifugo yenye tija kwa wafugaji na taifa kwa jumla.

Mhe. Kijaji amezindua shamba hilo Wilayani Kilosa Kijiji cha Mbwade Januari 3, 2025 wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku mbili Mkoani humo huku akisisitiza wafugaji na wakulima kuishi kwa amani na kila upande kuheshimu kazi ya mwenzake.

“…Mkoa wa Morogoro ni maalum kwetu ambayo inatakiwa kuwa mfano ndani ya taifa letu..." amesema Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji

Akifafanua zaidi, Waziri Kijaji amesema shamba hilo la malisho litakuwa la mfano hapa nchini ikiwa ni hatua madhubuti ya Serikali ya awamu ya sita kufanya mapinduzi ya sekta ya mifugo kwa kufuga kisasa ili kuwa na mifugo bora ambayo mazao yake ya yataweza kupelekwa katika masoko ya nje na kujipatia kipato hivyo kuondoa umaskini.

Sambamba na hayo, Mhe. Ashatu amewataka wananchi wa Mbwade na wa maeneo yote ya Mkoa huo kulinda na kutunza mazingira hususan vyanzo vya maji ili kuwa na maji ya uhakika ili kukidhi mahitaji ya wananchi wote na mifugo.

Akiwa katika shamba la kustawisha malisho la Kijiji cha Mandela Kata ya Magole Wilayani humo akizindua upandaji wa malisho ya mifugo aina ya Jun cao na Rhodes amewataka wafugaji kila mmoja kuwa na shamba lake la malisho sambamba na visima vya maji kwa ajili ya mifugo yake ili kuepuka ufugaji wa kuhama hama unaosababisha migogoro na ndugu zao wakulima.

Katika hatua nyingine, Waziri huyo amesema uchangiaji wa pato la taifa hapa nchini katika Sekta ya Mifugo imekuwa ikichangia kwa 7% hivyo ameahidi ifikapo mwaka 2030 uchangiaji wa pato la Taifa katika Sekta hiyo ufikie 10%.

Akimkaribisha Waziri kuongea na wananchi wa Kijiji cha Mbwade, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amemuomba Waziri kupata mbegu za malisho na mbegu za mifugo hususan Ng’ombe ili kupata mifugo yenye ushindani katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Aidha,  amewataka wafugaji kuwa na maeneo ya malisho kwani amesema kutokuwa na maeneo ya malisho ndio sababu kubwa ya uwepo wa  migogoro ya wakulima na wafugaji ambapo chanzo kikubwa ni wafugaji kulisha mashamba ya wakulima.

Naye, Chifu wa kabila la Wamasai Bw.  Matayani Simanga amemshukuru  Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wafugaji huku mfugaji Nyakungu Magairo wa Kijiji cha Mandela Kata ya Magole Wilayani Kilosa ambaye ana shamba la malisho amewashauri  wafugaji wenzake kuacha ufugaji wa kuhama hama badala yake wafuge kisasa kwa kumiliki mashamba ya malisho na visima vya maji.

Mwisho.



Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.