• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAZIRI MAKAME AMSHUKURU RAIS UJENZI WA SGR, MALIMA AWATAKA WAKAZI WA MOROGORO KUTUMIA FURSA HIYO.

Posted on: March 18th, 2024

Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mnyaa Mbarawa amemshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha za Ujenzi wa Reli ya kisasa ya Mwendo kasi – SGR ambayo inatarajia kuanza safari zake Mwezi Julai mwaka huu.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa (kulia) baada ya kuwasili na treni ya umeme kutokea Dar Es Salaam hadi Morogoro.

Prof. Mbarawa amesema hayo akiwa Mkoani Morogoro leo Machi 18, 2024 wakati wa majaribio ya awamu ya pili ya Reli hiyo ya mwendo kasi kutoka Dar es Salaam kuja Morogoro na kurudi Dar es Salaam ikiwa na mabehewa 14.

Amesema, Reli hiyo ni matunda ya Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye anafanya kila jitihada ya kupata fedha za ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Reli ya Mwendo kasi ambayo ameagiza ianze kufanya kazi ifikapo mwezi Julai mwaka huu.

“yote haya yamekuja kwa sababu ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa na leo tunaona matunda yake” amesema Prof. Makame Mbarawa.

Kwa upande wake Mkuu wa MKoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema kituo cha Kilosa cha reli hiyo ya mwendo kasi kitakuwa kiungo kikubwa kwa Uchumi wa Utalii ambapo amebainisha kuwa watalii wengi wanaokwenda Mbuga ya Wanyama ya Mikumi na Hifadhi ya Milima ya Udzungwa watakuwa wanashukia katika kituo hicho cha Kilosa.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima (kulia) akiongozana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania Masanja Kadogosa (kushoto)

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wakazi wa Mkoa huo na watanzania wote kwa jumla kuchangamkia fursa hiyo ya kutumia Reli ya mwendo kasi ambayo itasaidia kuwafikisha salama na haraka kutoka Morogoro Kwenda Dar es Salaam na maeneo mengine wanayotaka Kwenda.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro amewataka Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Morogoro kuangalia uwezekano wa kujenga miundo mbinu iliyo bora ya Barabara ya kuzunguka kituo cha Reli ya mwendo kasi cha Mjini Morogoro ili miundombinu hiyo ifanane na uwekezaji mkubwa alioufanywa na Mhe. Rais kwa kujenga kituo hicho Pamoja na eneo la kuhifadhia mizigo (Contener Terminar).

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania Masanja Kadogosa amesema Ujenzi wa Reli ya mwendo kasi wa kipande cha Dar es Salaam  hadi Morogoro umefikia asilimia 98.98 kazi kubwa iliyobakia ni ujenzi wa reli hiyo kuingia bandarini huku akibainisha kuwa ujenzi wa kipande cha Morogoro hadi Makutupora ya Singida umefikia asilimia 96.7.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.