• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waziri Mchengerwa aagiza Ujenzi wa hospitali kukamilika ndani ya siku 90

Posted on: May 20th, 2024

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Mohamed Mchengerwa (MB) amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ifakara Mji Bi. Zahara Muhidin Michuzi kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Afya TAMISEMI kuhakikisha wanakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji  Ifakara ifikapo Mwezi Agosti mwaka huu.

Waziri Mchengerwa ametoa agizo hilo leo Mei 20, 2024 ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake ya kutembelea miradi ya Maendeleo Mkoani Morogoro katika halmashauri za Ifakara Mji, Halmashauri ya Mlimba, Malinyi na Halmashauri ya Ulanga.

Amesema, hospitali hiyo inayojengwa kata ya kibelege imeshindwa kukamilika kwa wakati kutokana na  mivutano ya kisiasa, hivyo ametoa maagizo kuwa ifikapo Agosti Mosi, 2024 hospitali hiyo iwe imekamilika na wananchi wake kuanza kupata huduma za Afya.


Hata hivyo, ametumia fursa hiyo kuwaagiza watendaji nchi nzima kuacha mivutano na Wanasiasa na kusababisha ucheleweshaji wa miradi ya maendeleo, itampasa kuwachukulia hatua watendaji hao waliohusika ikiwa ni pamoja na kuwashusha madaraka yao.

Aidha, amesema, kwenye mivutano ya kisiasa wakiwemo Madiwani na kusababisha miradi mbalimbali ya maendeleo kusimama na kutokamilika kwa wakati atachukua hatua mara moja ikiwa ni pamoja na kusimamisha Baraza la Madiwani husika.

"...mnapovutana Wanasiasa na watendaji, watendaji wanashindwa kufanya maamuzi mnawanyima haki wananchi kupata huduma sasa tarehe 1/8/2024 nataka kuja kuzindua jengo hili..".ameagiza Waziri Mchengerwa.

Sambamba na maagizo hayo, amemtaka pia Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Ifakara Mhe. Kassim Faya Nakapala kuhakikisha anasimamia na kuondoa mvutano uliopo baina ya Madiwani na hospitali hiyo kukamilika kwa kipindi alichotoa, lengo ni kutowakosea haki wananchi wa Ifakara kwa kukosa huduma za matibabu ambayo ni haki yao ya msingi.

Awali, akimkaribisha Waziri, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima alimuomba Waziri Mchengerwa kumaliza Mgogoro uliopo wa kutokamilika kwa Hospitali hiyo ambayo Serikali imetoa fedha shilingi Bil. 1.5 lakini ujenzi huo umeshindwa kukamilika kwa zaidi ya miaka mitatu iliyopita na wananchi kuwanyima haki yao ya kupata matibabu kwenye hospitali hiyo.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.