• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAZIRI MKUU AONGOZA KIKAO CHA VIONGOZI MKOANI MOROGORO, KUJADILI MIKAKATI YA KUDHIBITI UHARIBIFU WA MAZINGIRA NA VYANZO VYA MAJI.

Posted on: December 24th, 2022

Kufuatia agizo la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alilolitoa Disemba 22 mwaka huu wakati wa uzinduzi wa ujazaji maji katika Bwawa la kuzalisha umeme la Mwalimu Julius Nyerere, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa ameitisha kikao cha kujadili viongozi mbalimbali wa serikali na wa kisiasa ili kujadili na kuweka mikakati ya kudhibiti uharibifu wa Mazingira na vyanzo vya maji Mkoani humo.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika kikao cha pamoja na Mawaziri wa Kisekta, Makatibu Wakuu na  Naibu Makatibu Wakuu, Viongozi wa Mkoa na Wilaya, Kamati za  Ulinzi na Usalama za Mkoa na wilaya za Morogoro  kujadili changamoto za usimamizi wa ardhi ndani ya mkoa  huo kwenye ukumbi wa Magadu katika Manispaa ya Morogoro,  Kushoto ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi,  Mhe. Mashimba Ndaki (Mb) na kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Angela Kairuki (Mb).

Viongozi mbalimbali wa ngazi ya Wilaya, Mkoa na hata Wizara wakiongozwa na Waziri Mkuu, wamekutana katika kikao kazi hicho kilichofanyika Disemba 24 mwaka huu katika ukumbi wa mikutano Magadu Mesi mjini Morogoro lengo kuu ni kujadili changamoto za utunzaji wa mazingira,  vyanzo vya maji na changamoto zinazoikabili sekta ya mifugo ambauo ndiyo Sekta inayotoa fursa kubwa za uchumi kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

Akizungumza wakati anafungua kikao hicho Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa amesema Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa mikoa 11 yenye changamoto ya uwepo wa mifugo mingi na migogoro mingi hapa nchini ikifuatiwa na mikoa ya Tanga, Iringa, Rukwa, Katavi, Tabora, Lindi, Arusha, Kigoma na Manyara. 

Mikoa hiyo imekuwa na changamoto ya kutokuwa na usimamizi mzuri katika sekta ya mifugo na hivyo kusababisha migogoro ya ardhi na ya wakulima na wafugaji.

Aidha, Mhe. Kassim Majaliwa  amesema changamoto hizo za mifugo mingi kuliko uwezo wa maeneo zina athiri mfereji unaopeleka maji katika bwawa la kuzalisha umeme la Mwalimu Julius Nyerere ambalo linategemewa kuzalisha umeme wa Megawati 2115.

Waziri Mkuu Majaliwa amesema kutokana na changamoto za mifugo kumeibuka tabia za ukatili ikiwemo mauaji, uharibifu wa vyanzo vya maji na mazingira, uharibifu wa mazao ya chakula pamoja na uharibifu wa hifadhi za misitu iliyohifadhiwa kisheria.

Sambamba na hilo Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amewataka viongozi kusimamia sheria, kanuni na taratibu ambazo nchi imejiwekea katika kutekeleza wajibu hivyo ni jukumu lao viongozi kila mmoja kwa nafasi yake kutambua nafasi yake.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Mhe. Lucas Lemomo amesema wao kama wawakilishi wa wananchi wameyapokea maelekezo yote ambayo Waziri Mkuu ameyatoa ya kuhakikisha kuwa maeneo yote yenye vyanzo vya maji yanalindwa, kutumia busara kwenye kutatua changamoto ya mifugo katika maeneo ya mabonde na kilimo na kutoa elimu kwa wananchi katika kila eneo kuhusu uvunajinmifugo.

Awali wakati akimkaribisha Waziri Mkuu, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma Mwassa amemshukuru Mhe. Kassim Majaliwa kwa ujio wake na kumthibitishia kuwa viongozi na wananchi katika Mkoa huo wapo tayari kupokea maelekezo ya utekelezaji ambayo Waziri Mkuu atayatoa katika kikao hicho huku akigusia namna Mkoa ukivyojipanga katika kulinda vyanzo vya maji kwa kuwaondosha wale wote wanaofanya shughuli za kibinadamu kwenye vyanzo hivyo lakini pia mkoa ulivyojipanga katika kuboresha sekta ya mifugo.

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.