• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAZIRI MKUU ARIDHISHWA NA UJENZI WA RELI YA MWENDOKASI.

Posted on: September 12th, 2021

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.  Kassim Majaliwa Majaliwa  amesema ameridhishwa na maendeleo ya  ujenzi wa kituo cha reli ya kisasa ya Mwendokasi - SGR kilichopo Kihonda katika Manispaa ya Morogoro.

Mhe. Kassim Majaliwa amesema hayo leo Septemba 12 mwaka huu wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa reli hiyo kutoka Dar es salaam hadi Kilosa Mkoani morogoro.

Amesema hadi sasa maendeleo ya ujenzi wa reli hiyo yanaridhisha kwa asilimia 99 hivyo wanatarajia kituo hicho kuanza kufanya kazi  kati ya Disemba mwaka huu  na Januari mwaka ujao.

‘’Tumeridhishwa na kazi inaendelea vizuri, na tukiwa tunaendelea na ukaguzi huu  ni lazima tuipongeze Wizara ya Ujenzi pamoja na Shirika lenyewe TRC’’ amesema Mhe. Majaliwa.

Aidha, Mhe. Kassim Majaliwa amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Morogoro  Martine Shigela kwa kuweka mikakati mizuri ya ujenzi wa kituo cha mabasi  katika stendi hiyo ya  SGR kwa lengo la kuwarahisishia abiria safari za kwenda mikoani na kumtaka kuendelea kusimamia ujenzi wa stendi hiyo.

Sambamba na hayo, amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando kutenga maeneo mahususi katika kituo cha reli ya mwendokasi kwa ajili ya Machinga ili kutowaruhusu kuzagaa katika maeneo ya kituo hicho.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amesema hadi sasa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro imeshatenga Shilingi Mil. 500 za ujenzi wa stendi hiyo ambayo itakuwa inahudumia abiria watakaofika katika stendi hiyo.

Pia, Shigela amesema stendi hiyo itapangwa maeneo ambayo yatawekezwa kwa ajili ya Hoteli pamoja na wafanyabiashara wadogo  ili wananchi wa Mkoa huo wafaidike na uwepo wa SGR katika Mkoa wa Morogoro.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando amesema amepoea maagizo ya Waziri Mkuu na kuahidi kusimamia ipasavyo maagizo hayo kwa kushirikiana na viongozi wa ngazi zote za Mkoa huo.

Akizungumzia suala la ujenzi wa makazi karibu na mradi huo, Msando amesema Manispaa itasimamia  vizuri mradi huo kwa kuzuia ujenzi holela katika maeneo ambayo mradi huo umepita kwa kuhakikisha majengo  yanayojengwa yanafuata kanuni na taratibu ambazo zimewekwa na Manispaa ya Morogoro.


Bonyeza link hii hapa chini utazame tukio hilo.

https://youtu.be/iMM287WewjE

MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.