• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waziri Mkuu aridhishwa na ujenzi wa stesheni Morogoro, asema itakuwa kitovu cha uchumi kwa wananchi.

Posted on: November 18th, 2020

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amekagua Kituo cha  Reli ya Mwendokasi (SGR) kinachoendelea kujengwa Kihonda Mkoani Morogoro na kusema kuwa ameridhishwa na ujenzi huo.

Kauli hiyo ya kuridhishwa na ujenzi huo ameitoa Novemba 18 mwaka huu alipotembelea kituo hicho ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu alipoteuliwa kwa mara ya pili na Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Waziri Mkuu kwa  awamu nyingine.

Mhe. Majaliwa amesema hayo mara baada ya kukagua Kituo hicho na kuwataka wakandarasi kukamilisha ujenzi huo kwa muda uliopangwa ili kuwasaidia  Watanzania kunufaika na uwepo wa Mradi huo.

“Mimi niwape taarifa, nimepita humu ndani nimeona kazi, nimeridhishwa na kasi ya Ujenzi huu, na sasa ndugu zetu wa Yapi Merkezi endeleeni kuchapa kazi kamilisheni mradi huu kwa muda ambao tumepangiana” amesema Mhe. Majaliwa.

Aidha, amesema reli ya mwendokasi  itakuza uchumi wa mtu mmoja mmoja kupitia biashara mbalimbali zitakazoendeshwa katika kituo hicho ambapo wafanyabiashara watapata fursa ya kusafirisha bidhaa zao kwa muda wanaoutaka.

Pia, Mhe. Waziri Mkuu amesema reli hiyo ilitakiwa kukamilika mwezi Disemba mwaka huu  lakini kutokana na janga la CORONA ilisababisha ujenzi huo kusimama huku akiwahakikishia Wananchi kuwa hadi mwezi April 2021 reli hiyo itaanza kufanya kazi.

Katika hatua nyingine, Mhe. Waziri Mkuu ameagiza Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na Jeshi la Magereza Mkoani humo kuwasilisha Nyaraka walizo nazo katika Ofisi yake ambazo zinaonesha umiliki wa eneo la Kilimanjaro Sisal lililopo Kihonda katika Manispaa hiyo ifikapo Novemba 28 ili kutambua uhalali wa eneo hilo ambalo kwa sasa pande hizo mbili hazijakubaliana juu ya umiliki wake.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amesema uwepo wa Reli ya Mwendokasi katika Mkoa wa Morogoro utatoa fulsa kwa wafanyabiashara, Wajasiliamali wadogo, wakulima na Wadau wengine kufanya biashara zao katika kituo hicho cha reli na kujiingizia kipato na hivyo kukuza uchumi wao.

Akizungumzia hatua ya ujenzi wa reli hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa, amesema pamoja na changamoto ya COVID – 19 kusababisha vifaa vya ujenzi huo kukwama kwenye nchi walikoagiza bado ujenzi wa kituo hicho umefikia zaidi ya asilimia 90.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo amesema kituo cha reli cha mwendokasi – SGR kitakuwa ndio kitovu cha biashara Mkoani humo huku akitoa wito kwa wananchi wa Morogoro kujiandaa namna watakavyofaidika na kituo hicho kwa kuwa hata nchi zilizoendelea stesheni huwa ndio maeneo muhimu ya biashara.

Aidha, ameitaka Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuweka uhusiano thabiti kati ya stesheni hiyo na maeneo mengine ya usafiri na usafirishaji kwa kuwa eneo hilo kwa sasa litakuwa mfano mahusus kwenye usafirishaji ndani ya Manispaa lakini pia kituo hicho kiwe dira ya Mji wa Morogoro kuelekea kuwa jiji.

MWISHO.


Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.