• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAZIRI MKUU ATOA MAAGIZO KURUDISHA MIUNDOMBINU YA BARABARA.

Posted on: April 16th, 2024

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amewataka Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini(TARURA) na Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) kuhakikisha wanarudisha miundombinu ya Barabara kwenye maeneo ambayo miundombinu yake imeharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha hapa nchini.

Mhe. Majaliwa ametoa maagizo hayo leo Aprili 16 alipofanya ziara ya siku moja Wiliyani Kilombero Mkoani Morogoro Tarafa ya Mlimba kwa lengo la kutoa pole kwa wahanga wa mafuriko ya Mvua zinazoendelea kunyesha na zilizosababisha athari kubwa katika kata ya Masagati na Utengule Wilayani humo na kuamua kwenda kujionea mwenyewe hali halisi ya athari hizo.

Akiongea na wananchi wa Mlimba katika Mkutano wa hadhara, Waziri Mkuu amewataka watanzania kuendelea kuwa wavumilivu na kuridhia Serikali iendelee kushughulikia maeneo yenye changamoto kubwa na baada ya mvua kupungua ndipo serikali itafanya kazi ya kubwa ya kurudisha miundombinu hiyo ya barabara katika hali yake.

Aidha, amesema serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan imeridhi kutoa mbegu tani 189 za mpunga, mahindi na alizeti kwa ajili ya waathirika wa mafuriko hayo ili waendelee na shughulia zao za kilimo mara baada ya mafuriko hayo kuharibu mazao mashanbani mwao

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Kighoma Malima amemuomba Waziri Mkuu Tsh. 1 Bil. Kwa ajili kufanyia matengenezo reli ya TAZARA baada ya reli hiyo kuharib8wa na maji ya mvua zinazoendelea kunyesha na kuacha inaning’inia hivyo mawasiliano ya usafiri huo kukosekana tangu  Aprili Mosi mwaka huu hivyo kusababisha adha kwa wananchi.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa kabla ya kumpokea Waziri Mkuu leo alikagua uharibifu wa  Reli hiyo ya TAZARA na kujionea hali halisi ya uharibifu uliopo na kutumia fursa hiyo kuwataka wananchi kuacha kufanya shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo na kukata miti kandokando mwa Reli hiyo ili kuondokana na adha ya uharibifu wa Reli na kuleta adha kwao na hasara kwa taifa.

Kwa upande wa waathirika na mafuriko ya mvua wa kata ya Masagati na Utengule Wilayani Kilombero amemwambia Waziri Mkuu namna Mkoa ulivyojizatiti kuwasaidia waathirika hao chakula na mahitaji mengine huku akibainisha kuwa changamoto kubwa kutofikika kwa wananchi hao  kwa kuwa wamezungukwa na maji hivyo akamuomba Waziri Mkuu usafiri wa Helikopta ili kuwapelekea chakula wananchi hao.

Kwa upande wake Regional Civil Eng. kutoka TAZARA Mhandisi James Mwasha amesema kwa tathmini iliyofanyika na kwa kasi iliyopo ya kurekebisha changamoto ya Reli hiyo kazi hiyo itakamilika ifikapo Aprili 28 mwaka huu na hasa kama watapata usaidizi wa kifedha.

Chakula ambacho kipo kwa ajili waathirika wa mafuriko hayo ya kata ya Masagati na Utengule ambcho hakijawafikia kwa sababu ya kutofikika ni Pamoja na Tani saba za mchele, kilo 350 za sukari, kilo 740 za maharagwe, lita 300 zamafuta ya kula na kilo 486 za chumvi

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.