• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waziri Mkuu awataka Madereva wa Serikali kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na maadili ya utumishi wa umma, atoa maagizo.

Posted on: October 24th, 2023

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akizungumza na Madereva wa Serikali wakati akifungua Kongamanon la siku tano la Chama cha Madereva wa Serikali Tanzania.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amewataka madereva wa serikali kufanya kazi zao kwa kufuata maadili ya utumishi wa umma na maadili ya kazi yao huku akibainisha kuwa madereva wana mchango mkubwa katika kutekeleza shughuli za serikali.

Mhe. Kassim Majaliwa amesema hayo wakati akifungua kongamano la siku tano la Chama cha Madereva wa Serikali Tanzania kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Morena iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ikiwa na lengo la kuwajengea uwezo madereva, kubadilishana uzoefu wa kazi sambamba na kujadili changamoto zinazowakabili.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akiwa pamoja na viongozi mbalimbali akwemo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima, Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Morogoro Mhandisi Masunga wakati wa kongamano la chama cha Madereva wa Serikali Tanzania.

"...ndugu washiriki mnatakiwa kuzingatia katika utendaji wenu wa kazi misingi na maadili ya utumishi wa umma, kuzingatia sheria za kazi na kuzingatia alama za barabarani..." amesema Mhe. Waziri Mkuu.

Aidha, Mhe. Waziri Mkuu amesema kufanya kazi kwa kufuata taratibu, kanuni, maadili na kuzingatia alama za barabarani kutasaidia kupunguza na kudhibiti ajali za barabarani ambao ndio mpango mkakati wa serikali wa kudhibiti ajali hizo na kutaka madereva wa serikali kuwa mfano kwa madereva wengine.

Sambamba na hilo, Mhe. Majaliwa amewataka waajiri serikalini kutatua changamoto zinazowakabili madereva, kuimarisha uhusiano na kuondoa migogoro isiyokuwa ya lazima maeneo ya kazi, kuweka mazingira mazuri ya kazi kwa kuwapa likizo madereva ili kupata muda wa kupumzika na hivyo kupunguza ajali zinazotokana na uchovu hivyo kuongeza ufanisi kazini.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akiwa pamoja na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya madereva wa Serikali baada ya ufunguzi wa kongamano la Chama cha Madereva wa Serikali Tanzania.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka    madereva hao kujiunga na mifuko ya pensheni ili baada ya kustaafu waweze kupata viinua mgongo na kusisitiza kuwa chama hicho ni muhimu kiwe na utaratibu unaofaa ili madereva wengi waweze kujiunga.

Kwa upande wake, Waziri wa ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa (Mb) amesema Serikali imefanya maboresho ya muundo wa kiutendaji ambao hapo awali kulikuwa na changamoto ya kupanda madaraja ambayo tayari serikali imekwisha tatua sambamba na kuwabadilishia madaraja madereva waliokuwa na sifa.

Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa (Mb) akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano la Chama cha Madereva wa Serikali nchini Tanzania.

Aidha, Mhe. Bashungwa amesema Wizara hiyo kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za utumishi wa umma zimejipanga kuhakikisha Chuo cha Usafirishaji (NIT) kitaendelea kutoa mafunzo bora kwa madereva na maafisa usafirishaji na kwamba Wizara itashirikiana vema na chama hicho kutatua changamoto zinazowakabili Madereva wa Serikali.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Ali Malima akitoa salamu za Mkoa amesema Serikali ya awamu ya sita imewafanyia mambo makubwa wananchi wa Morogoro na watanzania wote kwa jumla ikiwa ni pamoja na ujenzi wa reli ya mwendo kasi, ujenzi wa kiwanda cha Sukari cha Mkulazi na ujenzi wa bwawa la Kidunda ambalo linatarajiwa kuzalisha umeme zaidi ya Megawati 2000 hivyo kutatua kabisa tatizo la umeme hapa nchini.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akitoa salam za Mkoa wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Chama cha Madereva wa Serikali Tanzania.

Chama cha Madereva wa Serikali Tanzania (CMST) kiliazishwa Julai 7, 2013 na kusajiriwa mwaka 2015 kikiwa na malengo ya kuwaleta pamoja madereva wa Serikali, kutatua kwa pamoja changamoto zinazowakabili na kukemea matendo yanayoleta hasara kwa Serikali pamoja na kutetea Madereva kupata haki zao za kiutumishi.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.