• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAZIRI MKUU AZIAGIZA MAMLAKA ZA MIKOA NA WILAYA.

Posted on: March 5th, 2025



Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB), amezitaka Mamlaka za Serikali za Mikoa na Wilaya kuhakikisha zinabainisha vyanzo vya maji, kushirikisha wananchi wanaoishi karibu na vyanzo hivyo, na kuvipa ulinzi kwa kutunga sheria ndogo za kulinda vyanzo hivyo ili kuondokana na uharibifu wa vyanzo hivyo.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo Machi 5, 2025, wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa Bwawa la Kidunda, lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Mkoani humo ujenzi unalenga kuboresha upatikanaji wa maji katika mikoa ya Morogoro, Pwani, Dar es Salaam na baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Tanga.

Mhe. Majaliwa amesema ipo haja ya mamlaka hizo kutambua vyanzo vya maji katika maeneo yao ili kuweka mikakati ya kuvilinda na kuzuia uharibifu wa vyanzo hivyo kwa maslahi mapana ya Taifa na kusisitiza Mamlaka za Maji kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa kutunza vyanzo vya maji na kuwataka wakulima na wafugaji kuendelea kufanya shughuli zao pasipo kuathiri vyanzo hivyo.

"Nazitaka Mamlaka za Mikoa na Wilaya zifanye kazi ya kubainisha vyanzo vyote muhimu vinavyotiririsha maji na kutuletea maji kwenye maeneo yetu," amesisitiza Mhe. Kassim Majaliwa.

Sanjari na hayo, Waziri Mkuu amemtaka mkandarasi anayetekeleza mradi ws bwawa la kidunda kukamilisha kazi hiyo kwa wakati na kwa viwango vya ubora vinavyotakiwa huku akiwataka wananchi wanaozunguka mradi huo kuwa walinzi namba moja wa vifaa vinavyotumika katika ujenzi wa bwawa hilo ili kuhakikisha mradi huo unakuwa endelevu.

Katika hatua nyingine, Mhe. Majaliwa amewataka wananchi wa mkoa wa Morogoro kukomesha migogoro ya wakulima na wafugaji kwa kuishi huku wakiheshimiana kwa kuwa wote wanategemeana na kukemea tabia ya baadhi ya wafugaji kulisha mifugo yao mashamba ya wakulima na kwamba  jambo hilo kamwe halikubaliki.

Kwa upande wake, Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, amesema lengo la Serikali inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama, Hivyo ameitaka Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kutosubiri kukamilika kwa ujenzi wa bwawa hilo la Kidunda na kutoa wiki moja timu ya mamlaka hiyo iende Tarafa ya Ngerengere kuhakikisha wanatafuta maji kwa ajili ya wananchi wa Tarafs hiyo.


Naye Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, akitoa Salam za Mkoa amesema, hadi Februari 2025, wastani wa upatikanaji wa maji katika Mkoa wa Morogoro ni takribani 70% huku akibainisha kuwa Mkoa huo una miradi ya maji ya RUWASA yenye thamani ya shilingi bilioni 90, miradi ya maji ya MORUWASA ina thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 20, na miradi mingine ina thamani ya shilingi bilioni 75 na kwamba hiyo yote ni jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kumtua mwanamke ndoo kichwsni.

Ujenzi wa Bwawa la Kidunda ambao kwa sasa umefikia 28% hadi kukamilika kwake utagharimu zaidi ya shilingi bilioni 335, na utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu na unatarajiwa kukamilika Disemba 2026. Mradi huo unatekelezwa na Serikali Kuu kupitia Wizara ya Maji na kusimamiwa na Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA).


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.