• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waziri Ndumbaro aagiza wana Kilombero kutumia kampeni kutatua migogoro.

Posted on: December 15th, 2024



Waziri wa katiba na Sheria Mhe. Damas Ndumbaro ameagiza wananchi wa Wilaya ya Kilombero Mkoani Morogoro kutumia kikamilifu Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia kutatua migogoro inayowakabili hususan migogoro ya kijiji cha Utengule, Kambenga na Namhala.

Mhe. Ndumbaro ametoa agiza hilo Disemba 14, Mwaka huu wakati akizindua kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia "Mama Samia Legal Aid Campaign" katika kijiji cha Mkamba Wilayani Kilombero Mkoani humo ikiwa ni siku ya kwanza tu mara baada ya kampeni hiyo kuzinduliwa Kimkoa Disemba, 13, 2024.

"...naomba nikuagize ester na timu yako katika ziara hii ambayo tupo hapa wilaya ya kilombero msiondoke bila kwenda kwenye hayo maeneo matatu yenye mgogoro muongee na pande zote mjue kiini cha mgogoro ni nini ikiwashinda tuleteeni sisi taarifa mawaziri..." amesema Mhe. Dkt. Ndumbaro

Sambamba na hayo Mhe. Damas Ndumbaro amesema hifadhi ni maeneo ya watanzania wote kwa maslahi mapana ya nchi hivyo wanaovamia kwa maslahi yao binafsi watachukuliwa hatua kali za kisheria huku akiwaonya Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wanaochochea migogoro ya ardhi kwa kugawa maeneo hayo kiholela watafikishwa katika vyombo vya sheria na kupata adhabu wanayostahili.

Katika hatua nyingine, Waziri huyo ametembelea gereza la Kiberege na kusikiliza kero mbalimbali kwa wafungwa 15 na mahabusu 2 na kuwaahidi wafungwa hao kuletewa katika gereza hilo mifumo ya kidijitali kwa ajili ya kuhudhuria kesi zao kwa wale wanaokata rufaa baada ya hukumu wakiwa hapo gerezani bila ya wao kufika mahakamani.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe. Dastan Kyobya amebainisha migogoro iliyopo Wilayani humo kuwa ni pamoja na ile inayotokana na uvamizi wa misitu ya asili, migogoro ya ardhi, taraka, mirathi, mgawanyo wa mali na mashamba makubwa, mgogoro wa Kambenga, Mgogoro wa kijiji cha Namhala ambao hadi sasa una miaka 15 na mgogoro wa Kalenga kata ya Mofu.

Nao wananchi wa Kijiji cha Mkamba akiwemo Bi. Stamel Mlokota ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa maelekezo mahsusi na kuahidi kutekeleza kwa vitendo kampeni hiyo kwani amesema wananchi wa Wilaya hiyo wanakabiliwa na migogoro mingi ya ardhi, hivyo kampeni hiyo itawasaidia kutatua kero zao.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.