• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WAZIRI SILAA ATATUA MGOGORO KATA YA MLABANI

Posted on: July 8th, 2024

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Jerry Silaa (MB) ametatua mgogoro wa Ardhi wa muda mrefu baada ya wananchi wa Kata ya Mlabani kuvamia eneo lililokuwa linamilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Ifakara tangu mwaka 1938 ambapo Kanisa limekubali kupewa fidia ya eneo jingine ili wananchi hao waendelee na shughuli zao katika eneo hilo.

Makubaliano hayo yamefikiwa Julai 8, mwaka huu baada ya Waziri Jerry Silaa kuwasili Wilayani Kilombero na kufanya mazungumzo na Mmiliki wa eneo hilo lenye ukubwa wa zaidi ya hekali 500 ambaye ni Askofu wa Jimbo Katoliki la Ifakara Mhashamu Salutaris Libena na kukubali kupewa fidia ya eneo jingine.

Awali wakati akifafanua kuhusu mgogoro huo, Waziri Silaa amesema wananchi ndio wa Kata ya Mlabani ndio waliovamia eneo hilo linalomilikiwa na Kanisa Katoliki tangu mwaka 1938. hivyo Kanisa hilo linahitaji fidia ya kupewa eneo mbadala ili kulitumia katika shughuli zake mbalimbali zikiwemo ujenzi wa vyuo, hospitali na huduma nyingine za wananchi.

“…nimefika hapa Wilayani kwenu mahususi kwa ajili ya mgogoro wa Mlabani… nimekuja kwa ajili ya kumalizia makubaliano ambayo Mhasham Baba Askofu Libena kwa busara zake amekubali kupewa eneo jingine …” amesema Waziri Silaa.

Kwa sababu hiyo, Waziri Silaa ametoa siku 90 kwa viongozi wa Serikali na wataalamu kutumia ramani husika ili kupima na kupanga  eneo na baada ya kukamilika upimaji huo wananchi watalipia Tsh. 500 kwa mita moja ya mraba ili kupata hati ya eneo na kuwamilikisha ili kupata fedha za kununua eneo lingine la Kanisa hilo.


PiaMhe.  Jerry amewataka wananchi kutunza hati zao amesema za umiliki wa ardhi kwani ndio kielelezo cha juu cha umiliki ili kuacha kutapeliwa ardhi na kuondoa migogoro isiyo ya lazima.


Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mhe. Dunstan Dominic Kyobya amesema Wilaya hiyo ina maeneo mengi yenye migogoro ya ardhi yakiwemo Mlabani, Kambenga, Rubada huku akifafanua kuwa eneo hilo ala Mlabani mbalo linamilikiwa na Kanisa Katoliki la Ifakara lenye ukubwa wa zaidi ya ekari 500.


Katika hatua nyingine, Mbunge wa Jimbo la Kilombero Mhe. Abubakar Asenga amekiri kuwa eneo hilo ni la Kanisa ndio maana serikali imeshindwa kujenga shule, hospitali na vituo vya afya hivyo baada ya umiliki wa eneo hilo serikali itaweka utaratibu mzuri na kupanga mitaa ili kupata maeneo ya kujenga shule na kituo cha Afya.


Nao wananchi akiwemo Thomas Mwakilema Mkazi wa Mlabani amefurahishwa na ujio wa Waziri huyo na kukiri kuwa eneo hilo ni la Kanisa na kuahidi kutoa ushirikiano kutosha katika kulipia ili kupata hati ya umiliki na ameishukuru Serikali kwa kuwajali wananchi wake hususan kwa kutatua changamoto hiyo.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • Vyama vya Ushirika Vyatakiwa Kutumia TEHAMA

    May 14, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.