• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waziri Ulega akemea wavuvi haramu, atoa agizo TAWA.

Posted on: July 6th, 2023

Waziri wa Mifugo na uvuvi Mhe. Abdallah Ulega ameelekeza  Mamlaka ya usimamizi wa wanyamapori Tanzania (TAWA) kuwachukulia hatua kali za kisheria wavuvi haramu wanaofanya kazi hiyo bila kufuatia taratibu za uvuvi katika maeneo mbalimbali ya hapa nchini.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akizungumza wakati wa mkutano na wavuvi.

Mhe. Ulega ametoa maagizo hayo Julai 5, 2023 wakati wa mkutano na wavuvi uliofanyika katika Kata ya Kivukoni iliyopo Halmashauri ya Mji Ifakara akiwa katika ziara yake ya siku mbili katika Wilaya za Kilosa na Kilombero Mkoani Morogoro.

Amesema, wavuvi haramu huvunja kanuni, taratibu na sheria zinazotakiwa kufuatwa na wavuvi wote kwa kuharibu vyanzo vya maji na mazalia ya samaki, hivyo  kupunguza uzalishaji na mapato kwa serikali.

"...wapo watu wanaofanya uharibifu katika vyanzo  au mazalia ya wale samaki, wenyewe hayo mazalia mnayajua hivyo mnatakiwa kushirikiana na TAWA kudhibiti wavuvi haramu kwa manufaa mapana ya kwenu..."

Sambamba na hilo, Mhe. Ulega amesikitishwa na utitiri wa tozo unaowadidimiza wavuvi ikiwa ni pamoja na leseni 24000/=, kibali Tsh 15,000/=, kibali Cha siku Tsh 5000/=. Kwa sababu hiyo ameshauri kuwekwa gharama moja ili kuondoa kero ya malipo ya mara kwa mara kwani huo ni usumbufu kwa wananchi.

Kwa upande mwingine, Mhe. Ulega akizungumza katika mkutano huo wa hadhara amewataka wafugaji kutunza na kuthamini mifugo yao kwa kutafuta eneo maalum kwa ajili ya mifugo yao badala ya kulisha kwenye mashamba ya wakulima na kuiga mfano wa maisha ya wakulima wa kumiliki ardhi binafsi kwa ajili ya kilimo na kutaka wafugaji nao kumiliki ardhi binafsi kwa ajili ya malisho ya mifugo wao ili kuondoa migogoro baina ya jamii hizo mbili.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima (kushoto) akiwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega wakati wa mkutano na wavuvi.

Hata hivyo, Mhe. Ulega amesema wizara hiyo imejipanga kutoa hekta 10,000 eneo likilopo kata ya Mkata kwa ajili ya lunch itakayoitwa livestock guesthouse itakayochukua wafugaji wa muda mfupi ili kulisha mifugo yao huko.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema uvuvi haramu ni ukiukwaji wa kanuni, taratibu na sheria za uvuvi na kuhatarisha usalama wa hifadhi pamoja na viumbe waliomo  kwenye hifadhi hizo, hivyo ametoa wito kwa wavuvi hao kushirikiana na serikali kuwabaini waharifu hao Kwa maslahi mapana ya Kilombero, Mkoa wa Morogoro na nchi nzima kwa jumla.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akizungumza na wananchi wakati wa mkutano na wavuvi.

Naye, Kamishna msaidizi mwandamizi wa uhifadhi nyanda za juu kusini TAWA Joas Makwati amesema kwa sheria ya uhifadhi wa wanyamapori Tanzania ya mwaka 2009 hairuhusu shughuli za uvuvi katika eneo lililohifadhiwa ikiwemo mapori tengefu ya Kilombero lakini kutokana na umuhimu na uhitaji wa wananchi na Halmashauri kutaka kupata mapato, Wizara ya Maliasili na Utalii  mwaka 2020/21 iliruhusu wananchi kuingia kwenye maeneo hayo na kuweka utaratibu Maalum, huku akiwataka wananchi  kufuata kanuni na taratibu hizo.

Kamishna msaidizi mwandamizi wa uhifadhi wa wanyama pori nyanda za juu kusini  - TAWA Joas Makwati akizungumza na wananchi.

Nao wavuvi akiwemo Bw. Andrew Justine Mtolela ambaye ni Mwenyekiti wa kikundi Cha wavuvi amesema wanafanya kazi hizo kiasili kwa kuunga na sera ya serikali ya utunzaji wa mazingira ili kuongeza uzalishaji na mapato katika Halmashauri hiyo huku akithibitisha kuwa kuna baadhi ya wavuvi wakitumia njia haramu ambapo ameahidi watashirikiana na TAWA na Serikali katika kuwabaini waharifu wote haramu.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.