• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waziri Ummy Mwalimu Aagiza

Posted on: September 23rd, 2021

Waziri Ummy atoa wiki tatu Majengo ya nyongeza kutoa huduma kwa wananchi

Waziri wa Nchi OR – TAMISEMI Ummy Mwalimu ametoa wiki tatu kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro kuhakikisha majengo manne ya nyongeza yanayojengwa katika Hospitali ya Wilaya hiyo yanakamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.

Waziri Ummy Mwalimu ametoa agizo hilo leo Septemba 23 akiwa katika ziara yake ya siku moja Wilayani Mvomero ikiwa pia ni siku ya tatu tangu kuanza ziara yake Mkoani Morogoro na kutembelea ujenzi wa majengo hayo yanayojengwa kwa ajili ya kukamilisha miundombinu ya hospitali hiyo.

Baada ya kupata maelezo ya ujenzi huo, Waziri Ummy Mwalimu amesema katika kipindi cha Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali imeleta fedha kiasi cha shilingi Bilioni Moja kwa ajili ya kukamilisha majengo hayo ya nyongeza.

Hata hivyo Waziri Ummy Mwalimu ametoa Wito kwa viongozi wa Halmashuri hiyo kutaka kazi ya ujenzi wa majengo hayo kukamilika kwa wakati na wananchi wanapata huduma za afya mapema na kuagiza kazi hiyo imekamilika mapema na ifikapo Oktoba 15 mwaka huu huduma za Afya kwa wananchi zianze kutolewa.

“kazi ni nzuri nimeridhika nayo ila ninachotaka ikamilike haraka, tunakubaliana tarehe 15 Oktoba Mheshimiwa hizo huduma zianze kutolewa hapa” aliagiza Waziri Ummy Mwalimu.

Pamoja na maelekezo hayo Waziri alionekana ameridhika na kazi nzuri iliyofanyika katika kujenga majengo hayo, hivyo kuahidi kuleta fedha nyingine kiasi cha shilingi 300Mil. kwa ajili ya kujenga majengo mengine ya kipaumbele zikiwemo nyumba za Watumishi wa Hospitali hiyo ikiwa ni fedha za bajeti ya 2021/2022 iliyoanza Julai mwaka huu.

Katika hatua nyingine Waziri Ummy Mwalimu amesisitiza kuwa kila Halmashauri ijiwekee malengo ya kujenga miundombinu kwa kutumia fedha zinazotokana na makusanyo ya ndani kwa ajili ya kurudisha fadhila kwa wananchi kwa kuwajengea miradi ya maendeleo inayojielekeza kwenye huduma za kijamii kama maji, Zahanati, vituo vya Afya ama vyumba vya madarasa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela yeye pamoja na kuishukuru Serikali kuleta fedha za kutosha kwa ajili ya miradi mbalimbali Mkoani humo ameiomba Serikali kuiangalia kwa jicho la kipekee Hospitali ya Wilaya ya Mvomero kwa kuwa hospitali hiyo iko kwenye barabara Kuu ya kutoka Dar es Salaam kwenda Mji wa Serikali Dodoma, hivyo kuna changamoto za ajali za mara kwa mara zinatokea eneo hilo na kuiomba serikali kuongeza Vifaa tiba na wataalamu kwa maana ya madaktari bingwa kwa ajili ya kutatua changamoto hiyo inapotokea.

“ombi letu ni upatikanaji wa Wataalamu pamoja na vifaa ili hospitali yetu sasa iweze kufanya kazi inavyotakiwa hususan wakipatikana madaktari bingwa” amesisitiza Martine Shigela.

Mhe. Ummy Mwalimu amekamilisha ziara yake ya siku tatu Mkoani Morogoro kwa kutembelea shule ya Sekondari ya kumbukumbu ya Sokoine kwa kukagua ujenzi wa mabweni na Bwalo la chakula la wanafunzi yanayogharimu jumla ya shilingi 700 Mil. huku akionekana kutoridhishwa na matumizi ya fedha hizo na kuahidi kutuma timu ili  kuhakiki matumizi sahihi ya fedha hizo.

Halmashauri nyingine alizotembelea Waziri Ummy Mwalimu katika ziara yake ya siku tatu Mkoani hapa ni pamoja na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.