• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wizara ya Sheria kuanza kampeni ya msaada wa kisheria Mkoani Morogoro.

Posted on: December 10th, 2024



Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushirikiana na Mkoa wa Morogoro, inatarajiwa kuanza Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kwa lengo la kusogeza karibu huduma hiyo ikiwemo utoaji wa Elimu inayohusu masuala ya haki na sheria na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wa Mkoa huo.


Kampeni hiyo inatarajiwa kuzinduliwa rasmi Disemba 13, Mwaka huu katika eneo la stendi ya daladala ya zamani iliyopo Manispaa ya Morogoro  na baada ya uzinduzi wa kampeni hiyo itaendelea kufanyika katika Halmashauri zote za Mkoa huo kwa siku 10 mfululizo ikiwa na lengo la  utoaji elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kisheria kama vile Ardhi, Haki za Binadamu na Utawala Bora, Mirathi, Ndoa, Ukatili wa Kijinsia, Madai, Jinai vilevile itahusisha huduma ya usajili na utoaji vyeti vya kuzaliwa na kifo vitakavyotolewa na RITA.


Ratiba iliyotolewa inaeleza kuwa, mara baada ya uzinduzi huo kampeni itaendelea kwenye  ngazi ya Halmashauri ambapo itafanyika kwa kata 10 na vijiji 30 kwa kila Halmashauri ikigusa moja kwa moja kutatua  changamoto za wananchi hususan masuala ya kijinsia, migogoro ya ardhi, mirathi na utoaji wa Elimu ya haki za binadamu kwa ujumla.


Kampeni hiyo ya Mama Samia inaongeza uelewa wa kisheria na haki za binadamu ndani ya jamii ikiwemo haki za wanawake na watoto, huduma ya  ushauri  wa kisheria na unasihi kwa waathirika wa ukatili wa kijinsia pia kuongeza uelewa kwa wananchi kuhusu wajibu na misingi ya utawala bora.


Kampeni hiyo inachangia uboreshaji na upatikanaji wa haki kwa makundi mbalimbali wakiwemo wanawake, watoto na makundi mengine yaliyo katika mazingira hatarishi pamoja na kuimarisha amani na utulivu, kuongeza kipato na  kuleta utengamano wa kisiasa hapa nchini.


Ikumbukwe kuwa Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa Mikoa yenye migogoro lukuki inayohusu ardhi na migogoro mingine, hivyo, wananchi mnaombwa kushiriki kwenye kampeni hiyo na kushiriki kwa wingi ili wataalam waliopo kwenye kampeni hiyo waweze kutatua kero na migogoro inayowakabili.


Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.