• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

ZAIDI YA BIL. 41 KUKAMILISHA UJENZI WA MAJENGO 7 SUA

Posted on: November 14th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amethibitisha majengo 7 kujengwa na mengine kufanyiwa ukarabati ambapo itagharimu zaidi ya Tsh. Bil. 41 katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kampasi ya Morogoro kupitia mradi wa Elimu ya Juu  kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) ili kuongeza idadi ya majengo kwa ujifunzaji na ufundishaji wa wanafunzi na wataalam mbalimbali ya kilimo.


Mkuu huyo wa Mkoa ametoa kauli hiyo Novemba 14, Mwaka huu katika hafla ya utiaji Saini wa mikataba ya ujenzi wa majengo ya chuo cha SUA iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo hicho yakilenga kuboresha mazingira ya kujifunzia.

Aidha, Mhe. Adam amesema mradi huo utatekelezwa ndani ya miezi 18 pekee na majengo hayo kukamilika kwa ajili ya utoaji huduma ya elimu, hivyo amewataka wakandarasi waliotia saini ya kutekeleza mradi huo kufuata maelekezo ya mikataba na kuhakikisha majengo hayo yanakamilika kwa wakati huku akifurahishwa na wakandarasi wazawa waliotia saini ya mkataba wa ukarabati wa majengo chakavu ya chuo hicho.

“… sote tumeshuhudia utiaji saini wa mikataba ya ujenzi wa majengo 7 ambapo jumla yake inagharimu Tsh. Bil. 41.05 kukamilisha majengo hayo…” amesema Mhe. Adam Kighoma Malima

Katika hatua nyingine, Mhe. Malima amesema chuo hicho kinapaswa kuwa mfano Afrika katika shughuli za kilimo kwa kutumia maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa  kufanya mageuzi ya kilimo hapa nchini kwa kuanzia Mkoani humo kuzalisha kutafuta ufumbuzi wa mazao ya kimkakati hususan karafuu, michikichi, parachichi, kokoa na hiriki kwani kilimo ndio uti wa mgongo hapa nchini.

Sambamba na hilo, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka watumishi wa umma pamoja na wananchi waliojiandikisha katika orodha ya daftari la serikali za mitaa kujitokeza kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa ambao utahusisha wenyeviti wa mitaa, vitongoji na vijiji ifikapo Novemba 27, Mwaka huu.

Kwa upange wake, Mwakilishi wa Mradi wa HEET Mhandisi Hanington Kagiraki akimwakilisha mratibu wa HEET kitaifa amewahakikishia wakandarasi kuhusu fedha zote za mradi huo zimetayarishwa hivyo hakutakuwa na sababu za kutokamilisha mradi huo kwa wakati.

Naye, Makamu Mkuu wa Chuo cha SUA Prof. Raphael Chibunda amesema kukamilika kwa mradi huo itasaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia na kuboresha miundombinu ya kutolea elimu kwani chuo hicho ndio tegemezi katika masuala mbalimbali ya kilimo hapa nchini.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.