• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

Posted on: March 4th, 2021

Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro inatarajia kutumia  zaidi ya Shilingi Bil. 7 kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ambazo zitatumika kwa ajili ya mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa miradi ya maendeleo Mkoani humo.

Hayo yamebainishwa na Mchumi Mwandamizi Emmanuel Mazengo leo Machi 3 mwaka huu katika kikao cha baraza la wafanyakazi cha Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro kilichofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kilicholenga kupitisha mipango na bajeti ya mwaka wa fedha 2021/2022.

Mazengo amebainisha kuwa bajeti hiyo imejikita katika matumizi ya kawaida na matumizi ya maendeleo ambayo yatahusisha mishahara  kwa wafanyakazi na maslahi ya watumishi.

Aidha, Mazengo amesema kwa upande wa fedha za matumizi ya maendeleo miradi itakayoendelezwa ni pamoja na zaidi ya shilingi Bil. 2.5 zitatumika kwenye ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Fedha nyingine zitatumika kwenye Ujenzi wa Ofisi za Wakuu wa Wilaya za Gairo, Ulanga na Malinyi lakini pia fedha hizo zitatumika katika ujenzi wa Ofisi 10 za Maafisa Tarafa zitakazogharimu shilingi milioni 700.

Akifungua kikao hicho Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo, amewataka Wakuu wa Idara, wakuu wa sehemu/vitengo na watumishi wengine kutoa kipaumbele katika kuhakikisha watumishi  wanapata stahiki zao kwa mujibu wa sheria, kanuni, taratibu na miongozo kwa mujibu wa maeneno yao ya kazi.

Mhandisi Kalobelo amesema  pale ambapo itaonekana kuna tatizo katika kuwapa stahiki zao kwa wakati ni vyema kutoa ushirikiano kwa kuwaeleza sababu ambazo  zimepelekea kikwazo cha kutowapa stahiki zao ili kuepuka migogoro baina ya wafanyakazi.

‘’Niwaombe sisi tuliopo hapa wengine ni wakuu wa idara, wengine ni wakuu wa sehemu/vitengo lakini na watumishi wengine, niombe twendelee kutoa kipaumbele katika kuhakikisha kwamba watumishi wanapata stahiki zao kama inavyotakiwa kisheria, kanuni, taratibu na miongozo ya maeneo yetu ya kazi’’ amesisitiza Kalobelo.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Kalobelo amewataka Wakuu wa Idara na Makatibu Tawala wa Wilaya kuepuka malimbikizo ya madeni kwa kuweka mipango mikakati kulingana na pesa wanazopata kikamilifu kila mwezi kutoka Serikali kuu OC hivyo watumie pesa hizo kwa kuzingatia vipaumbele vya mahitaji ya Ofisi zao ili kuepukana na madeni.

Sambamba na hayo, Mhandisi Kalobelo ametoa wito kwa wadau wa kikao hicho kuwa wawezeshaji wa kutekeleza miradi ya maendeleo ambayo ipo katika maeneo yao ikiwa ni pamoja na miradi kutoka Serikali kuu na miradi ya Serikali za mitaa.

Akibainisha malengo ya  kikao hicho Afisa Elimu wa Mkoa wa Morogoro Bi. Joyce Baravuga amesema ni kuangalia maendeleo  na ustawi wa wafanyakazi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro na kupitisha mipango na bajeti ya mwaka 2021/2022 ili ipelekwe Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Aidha, Bi. Baravuga amesema  amepokea maelekezo ya mwenyekiti wa kikao hicho Katibu Tawala wa Mkoa huo Mhandisi Emmanuel Kalobelo katika kuzingatia suala la kujali stahiki za watumishi wa chini yao na akatumia fursa hiyo kuwataka viongozi wa chini yake hususan walimu kusimamia vema mifumo ya elektoniki iliyopo katika shule za Msingi na Sekondari ikiwa ni utekeleaji wa maagizo ya mwenyekiti wa kikao hicho.

Naye, Katibu Tawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Yohana Kasitila ametoa kongole kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo kwa jitihada kubwa ambazo anazifanya katika kuleta maendeleo katika Mkoa huo, kisha ametoa ombi la kujengewa nyumba au kufanyiwa ukarabati kutokana na miundombinu ya nyumba hiyo kuwa mibovu.


MWISHO.



Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.