• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

Posted on: May 18th, 2025

Zaidi ya shilingi Tsh. Milioni 125 zimepatikana  kupitia chakula cha hisani ambapo ilifanyika harambee ya kupata fedha kwa ajili ya  maboresho ya miundo mbinu ya Hospitali ya Rufaa ya Morogoro ambayo jana Mei 17 imetimiza miaka 80 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1945.

Harambee hiyo iliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Alhaji Adam Kighoma Malima ambaye alikuwa mgeni Rasmi kwenye hafla hiyo iliyofanyika Hoteli ya Morena Manispaa ya Morogoro ambapo wadau mbalimbali wa ndani na nje ya Mkoa huo walichanga fedha taslim na wengine kutoa ahadi na kufikisha kiasi hicho huku Mkuu wa Mkoa naye akiahidi kutafuta Mil. 10

...kwa harambee iliyosomwa leo ningependa isomwe milioni 125 Mkuu wa Mkoa anaenda kujipiga atatoa Tsh. Milioni 10..."  amesema Mhe. Adam Malima

Akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro pamoja na wageni waalikwa walioshiriki maadhimisho hayo ya Kilele cha miaka 80 ya Hospitali hiyo Mhe. Kighoma Malima alitumia fursa hiyo kuwapongeza watumishi wa Hospitali hiyo ya Rufaa kwa kufanya kazi kwa bidii na nje ya changamoto zozote wanazokutana nazo.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo Dkt. Best Magoma amesema Sekta ya afya kwa Mkoa wa Morogoro iko vizuri kutokana na kuwa na Madaktari wenye weledi, wabobevu na wansojituma katika utoaji wa huduma za afya kwa wananchi.

Naye, Dkt. Lita Lyamuya Mganga Mfawidhi mstaafu wa Hospitali hiyo amesema hali iliyopo katika Hospitali hiyo kwa sasa ni nzuri huku akisisitiza kuendeleza ushirikiano na wadau mbalimbali katika kuhakikisha wanatoa huduma bora na yenye kukidhi matarajio ya Serikali na wananchi.

Harambee hiyo ililenga kupata fedha za ukarabati wa miundombinu ya Hospitali hiyo ya Rufaa pamoja na kununulia vifaa tiba kama jitihada za kuunga mkono Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • Zaidi ya Mil. 125 zachangwa kupitia chakula cha hisani kukarabati Hospitali ya Rufaa Morogoro.

    May 18, 2025
  • RC MALIMA ASHIRIKI MATEMBEZI YA HISANI, ASEMA HOSPITALI YA RUFAA INAHIMILI WAGONJWA.

    May 17, 2025
  • VYAMA VYA SIASA NCHINI VYATAHADHARISHWA

    May 15, 2025
  • RC MALIMA ATAKA VYAMA VYA USHIRIKA VYA WAFUGAJI

    May 15, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.