• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Zaidi ya Tsh. 900 Bil. zatengwa Mkoani Morogoro kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo.

Posted on: March 7th, 2025


Mkoa wa Morogoro umepanga kutumia kiasi cha shilingi trilioni 1.3 kwa mwaka wa fedha 2025/2026 kati ya fedha hizo kiasi cha shilingi 946.7 Bil. kimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyopangwa kutekelezwa Mkoani humo kwa mwaka huo wa fedha.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, Machi 6, 2025 wakati wa kikao cha 43 cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Magadu Manispaa ya Morogoro kikilenga kujadili mwenendo wa mpango na bajeti ya Mkoa kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Akifafanua zaidi, Mhe. Malima amesema kuwa kiasi cha shilingi 389.9 zitatumika kwa ajili ya mishahara ya watumishi wa umma na matumizi mengine ya kawaida.

 "Katika mapendekezo ya bajeti ya mwaka 2025/2026, Mkoa wa Morogoro unakadiria kutumia jumla ya shilingi trilioni 1.3 kwa ajili ya miradi ya maendeleo na matumizi mengine ya kawaida," amesema Mhe. Malima.

Mhe. Adam Malima ametumia kikao hicho kuwakumbusha watumishi wa umma ndani ya Mkoa huo kushiriki shughuli za kijamii, ikiwa ni pamoja na maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani na kushiriki kikamilifu maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yatakayofanyika kimkoa Machi 8, 2025, katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara.

Kwa upande wake, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, amesisitiza umuhimu wa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo, hasa ile inayogusa wananchi wa hali ya chini kama shule, zahanati na vituo vya afya.

Naye, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Joseph Masunga, ameipongeza Serikali ya Mkoa huo kwa juhudi za kuimarisha mahusiano baina ya wakulima na wafugaji, hali iliyosaidia kupunguza migogoro ya pande hizo mbili, hata hivyo amesisitiza kuongeza jitihada katika kutatua migogoro ya ardhi kati ya wananchi na hifadhi pamoja na migogoro baina ya wananchi na taasisi za umma.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.