• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Zaidi ya Tsh. Bil 347 kutekeleza miradi ya kitaifa Mkoani Morogoro.

Posted on: January 8th, 2025



Zaidi ya shilingi Bil.347 zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza ujenzi wa miradi mikubwa ya kitaifa Mkoani Morogoro ikiwemo mradi wa Ujenzi wa barabara ya Bigwa – Kisaki Mkoani humo.

Hayo yamebainishwa na Meneja wa TANROARDS Mkoa wa Morogoro Mhandisi Lazeck Kyamba Januari 7, Mwaka huu wakati wa kikao cha 42 cha Bodi ya Barabara kilichofanyika katika ukumbi wa Magadu uliopo Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

“...Mheshimiwa mwenyekiti Mkoa wa Morogoro una miradi mitano mikubwa ya kitaifa ukiwemo mradi ujenzi wa barabara ya Ifakara – Kihansi mpaka Mlimba, Taweta Madeke  Sehemu ya Ifakara hadi Mbingu ..” Amesema Mhandisi Lazeck Kyamba. 

Akifafanua zaidi, Mhandisi Kyamba amebainisha miradi hiyo inayoendelea kujengwa Mkoani humo ni pamoja na mradi wa barabara ya Bigwa – Kisaki wenye thamani ya Tsh. Bil 132, mradi wa barabara ya Ifakara - Kihansi – Mlimba – Taweta - Mbingu yenye thamani ya Tsh. Bil. 97.2, 

Mradi mwingine ni mradi wa barabara ya Ubena Zomozi – Ngerengere itakayogharimu kiasi cha Tsh. Bil 20.5, mradi wa barabara ya Ifakara - Kihansi – Mlimba – Taweta sehemu ya Ifakara – Mbingu - Chita utagharimu kiasi cha Tsh. Bil 70.8, lakini pia mradi wa ujenzi wa barabara ya kuingia kwenye vituo vya kushushia na kupakia mizigo na abiria vya treni ya kisasa ya SGR.

Aidha, Mhandisi huyo amesema kumekuwa na uharibifu mkubwa wa miundombinu hususan makaravati, barabara na madaraja hivyo serikali ngazi Mkoa iliidhinishiwa na Serikali Kuu kiasi cha Tsh. Bil. 20.7 kwa mwaka wa fedha 2024/2025 ili kufanya matengenezo ya kudumu ya miundombinu ya barabara na bajeti ya Tsh. Bil 3.5 zikiwa fedha za miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima amesema serikali imejipanga kupunguza ajali za barabarani Mkoani humo kwa kushirikiana na jeshi la polisi huku akisisitiza kujiandaa kuwekeza kwenye matumizi ya mifumo ya kidijitali ikiwemo kufunga ta ana kamera za barabarani ili kutambua makosa yanayofanywa na baadhi ya madereva wasiozingatia sheria za barabarani .

Katika hatua nyingine, Mhe. Malima amekemea vikali tabia ya baadhi ya wamiliki wa magari  ambao magari yao yakiharibika yanaegeshwa barabarani na hata kufanyiwa wengine kudiliki kufanyia matengenezo ya magari hayo barabarani badala ya kuyavuta na kuyaweka mahali salama na kwamba watachukua hatua kwa wamiliki wenye tabia hiyo. 

Naye, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mhe. Innocent Kalogeresi ameshauri Serikali iongeze bajeti ya fedha za TARURA na TANROADS Mkoani humo ili kukidhi haja ya kutengeneza miundombinu ya Mkoa huo kwa sababu ni mkoa mkubwa na unam aji mengi yanayoharibu miundombinu.

Kwa upanade wake Mbunge wa Malinnyi Mhe. Antipasi Mgungusi ameiomba Serikali kukamilisha kivuko cha Kikove ili wananchi wa Malinyi na Mlimba kupata urahisi wa kusafiri kwenda Mkoani Songea badala ya kuzunguka kupitia Mkoa wa Iringa.



Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.