• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

ZAO LA KARAFUU SASA KUSOMESHA WANAFUNZI ELIMU YA JUU MOROGORO.

Posted on: February 26th, 2025


Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt.  Mussa Ali Mussa ametoa miche 10 ya mikarafuu kwa kila mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule ya Sekondari Kisemu iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya  Morogoro Mkoani humo kama ishara ya kuendeleza Kampeni ya Jisomeshe na Mkarafuu katika Mkoa huo.

Dkt. Mussa amegawa miche hiyo February 25, Mwaka huu wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi ya usambazaji endelevu wa maji vijijini na usafi wa mazingira (SRWSS) katika vituo vya afya vya Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro na shule hususan ujenzi wa vyoo.

Aidha, Dkt. Mussa amewataka wataalam wa kilimo kutembelea shule hizo na kutoa Elimu ya kustawisha zao la karafuu kwa wanafunzi ili kusaidia kutunza miche ili liweze kuwa tija kwao na kwa wazazi hivyo kusaidia gharama ya watoto hao katika kupata Elimu kupitia zao hilo la karafuu.

Amesema kampeni hiyo ya JISOMESHE NA MKARAFUU inalenga  wanafunzi wa kidato cha kwanza kupanda miche hiyo ili kuwanufaisha  wanafunzi kwa kujisomesha wenyewe  kupitia zao la karafuu na kukuza kipato cha familia zao, lakini pia kutunza mazingira katika ngazi ya Mkoa na Taifa kwa ujumla.

“…mikarafuu hii mtaweza kukaa nayo kwa miaka 4 kisha itaanza kuzaa mtakapofika kidato cha nne kabla ya kufanya mtihani basi itaanza kuzaa na kila mkarafuu utazaa sio chini ya kilo 5” amesema Dkt. Mussa 

Aidha, Kampeni hiyo ni moja wapo ya hatua za utekelezaji wa ajenda ya kilimo ifikapo 2030 huku wakiendelea kukuza kipato kinachotokana na mazao ya viungo kwani mazao hayo ni mazao ya kimkakati katika Mkoa wa Morogoro ikiwemo zao la parachichi, Kakao, Mchikichiki na karafuu yenyewe.


MWISHO.

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI. May 13, 2025
  • View All

Habari Mpya

  • MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI KUFANYA KAZI ZAO KIMKAKATI.

    May 26, 2025
  • MWAROBAINI WA CHANGAMOTO YA MAJI MOROGORO HII HAPA, RC MALIMA ATOA MAAGIZO.

    May 24, 2025
  • UZALISHAJI WA MAZIWA KUCHANGIA BIL. 18 KWA MWAKA MOROGORO

    May 23, 2025
  • MAAFISA HABARI TOENI UFAFANUZI DHIDI YA UPOTOSHAJI- MCHENGERWA

    May 23, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.