• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Mlimba
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za Ugavi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

ZIARA YA WAZIRI BASHUNGWA

Posted on: July 23rd, 2022

Waziri Bashungwa akagua miradi ya maendeleo Kilosa aacha maagizo mazito

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Innocent Lugha Bashungwa amefanya ziara ya kikazi ya siku moja Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro ziara iliyolenga kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa Wilayani humo huku akiacha maagigo mazito yanayotakiwa kutekelezwa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa (MB) Innocent Bashungwa akiongea na wafanya biashara ndogo ndogo (hawapo pichani) wa eneo la Mtumbatu Wilayani Kilosa alipofanya ziara ya siku moja wilayani humo

Waziri Bashungwa amefanya ziara hiyo Julai 23, 2022 na kutembelea miradi mitatu ikiwemo ujenzi wa Sekondari ya Belega ambayo imepelekewa shilingi Bilioni Moja, ujenzi wa Daraja la Belega lenye Urefu wa mita 140 ambapo hadi kukamilika kwake litagharimu zaidi ya shilingi 7.9 Bil. Pamoja na Kituo cha Afya cha Nhembo ambacho nacho kimepelekewa shilingi milioni 700.

moja ya majengo ya sekondari ya Belega wilayani Kilosa ambayo Waziri Bashungwa ameyatembelea.

Akiwa katika Sekondari ya Belega amemuagiza Mkuu wa MKoa  huo Martine Shigela kusimamia kamati mbili zilizoundwa kuangalia matumizi ya fedha Shilingi Bilioni Moja zilizoletwa na Serikali katika shule hiyo kwa ajili ya kidato cha tano na cha sita kama matumizi yake yamefuata taratibu na miongozi iliyopo na kumtaka kuwasilisha  taarifa ya kamati hizo  haraka Ofisini kwake.

“nimemuelekeza Mkuu wa Mkoa kwa utaratibu ambao tayari umeutoa, sasa lipe msukumo, timu ifike tujiridhishe kama Bilioni moja ambayo mheshimiwa Rais amewezesha wananchi wa Jimbo la Kilosa Kupitia kwa Mbunge Mhe. Profesa Kabudi kama tumepata matumizi halisi ya hiyo Bilioni moja” aliagiza Waziri Bashungwa.



Waziri wa TAMISEMI Innocent Bashungwa (wa pili kushoto) akikagua ujenzi wa majengo ya shule ya sekondari Belega Julai 23 mwaka huu. kushoto ni DED wa Halamshauri ya Wilaya ya Kilosa Kisena Mabuba na kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Majid Mwanga na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela

Katika Hatua nyingine amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Kisena Mabuba kuhakikisha watoto wa kidato cha tano wanaotarajia kuanza hivi karibuni kuanza kutumia vyumba vya madarasa ya shule hiyo yanayoendelea kukamilishwa sasa. 

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Belega.

 

Akiwa katika mradi wa ujenzi wa Daraja la Berega ambalo limewakosesha wananchi wa kata ya Belega mawasiliano kwa muda mrefu na hata kusababisha vifo vya wakazi wake amemtaka mkandarasi anayejenga daraja hilo lenye urefu wa mita 140 Nyanza Road Works Ltd kukamilisha kazi hiyo ifikapo mwezi Juni 2023 kama mkataba unavyoonesha.

Hili ndo Daraja la Belega ambalo linalotumika kwa sasa, ambalo ni hatari kwa wananchi wakati wa masika.

Maagizo hayo ameyaelekeza pia kwa Meneja wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini TARURA Mkoa wa Morogoro Mhandisi Benjamin Maziku kusimamia ukamilishaji wa mradi huo kwa muda uliopangwa na si vininevyo.

Aidha, amemuagiza Meneja huyo wa TARURA Mkoa wa Morogoro kuanza kufanya utafiti wa kufanyia matengenezo maeneo yasiyopitika kiurahisi barabara hiyo ambayo inaunganisha Wilaya ya Kilindi Mkoani Tanga ili yaboreshwe na daraja hilo kuwa na tija kwa wilaya nne za Kilosa na Gairo za Mkoa wa Morogoro na Kilindi na Handeni kwa Mkoa wa Tanga.

Waziri Bashungwa (wa pili kushoto) pamoja na ujumbe wake wakiangalia ujenzi wa Daraja jipya. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Martine Shigela, Kushoto kwake ni Mbunge wa Jimbo la Kilosa Prof. Mhe. Palamagamba Kabudi na kulia ni Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro, Mhandisi. Ezron Kilamhama.

Mwonekano wa ujenzi wa Daraja jipya la Belega.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela akifafanua kuhusu hatua zilizokwisha chukuliwa juu ya ujenzi wa shule ya sekondari ya Belega amesema zimeundwa timu mbili moja inahusika na ukaguzi (Auditing)kujiridhisha kama manunuzi ya vitendea kazi yalifuata kanuni na taratibu, kamati nyingine ni ile takayojikita upande wa utalaam wa uhandisi.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Martine Shigela wakifurahia jambo na Waziri Bashungwa, Kushoto ni Katibu wa CCM wilaya ya Kilosa.

Amesema timu zote hizo mbili zinatarajia kuanza kazi Julai 25 2022, na kwamba wajumbe wa kamati hizo watatoka TBA, TEMESA, National Housing, Wataalamu kutoka ngazi ya Mkoa pamoja na vyombo vya Ulinzi na Usalama.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kilosa Mhe. Profesa Palamagamba Kabudi ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha fedha za miradi hiyo jimboni kwake hususan ujenzi wa Daraja la Belega ambalo ni muhim sana kwa wananchi wa Kata ya belega kwani amesema daraja hilo limekuwa kero kwa wananchi wake kwa muda mrefu.

Waziri wa TAMISEMI Mhe. Innocent Bashungwa akipokea zawadi ya mbuzi kutoka kwa wakazi wa kata ya Nhembo, mara baada ya kukagua ujenzi wa kituo cha Afya cha Nhembo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kilosa Prof. Mhe. Palamagamba Kabudi, akishuhudia tukio hilo.

Huku Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro Mhandisi Benjamin Maziku akibainisha kuwa mradi huo wa barabara unatekelezwa kwa miezi 18 kuanzia Disemba 21, 2021 uliposainiwa hadi Juni 20, 2023 na kwamba gharima ya mradi hadi kukamilika ni shilingi 7,905,122,445.65 (bila VAT) hadia na kwamba ujenzi wa daraja hadi sasa umefikia asilimia 13.7

Waziri Innocent Bashungwa akikamilisha ziara yake ya siku moja Wilayani Kilosa kwa kutembelea ujenzi wa Kituo cha Afya cha Nhembo kilichopo kata ya Mabula na kuwapongeza wananchi wa kata hiyo kwa kushiriki kikamirifu katika ujenzi wa kituo hicho cha Afya.

 

Waziri Bashungwa ampongeza mmoja wa wazee walioshiriki kikamilifu katika ujenzi wa kituo cha Afya Nhembo.

MWISHO 

 

Matangazo

  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2024 October 30, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • RC MALIMA AKEMEA ULANGUZI WA MAZAO.

    May 08, 2025
  • WAAJIRI MOROGORO WATAKIWA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYA KAZI WAO.

    May 01, 2025
  • SERIKALI KUJENGA BARABARA YA LUPILO – MALINYI KWA KIWANGO CHA LAMI, Bil. 18 ZATOLEWA KUJENGA MADARAJA MAWILI.

    April 25, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATAJA TUNU NNE ZA TAIFA.

    April 19, 2025
  • View All

Video

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Kighoma Malima akikagua ujenzi wa jengo la ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro

    Sanduku la Posta: S.L.P 650 MOROGORO

    Simu: +2550232934305

    Simu: +255766828252

    Barua pepe: ras.morogoro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2024 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.